Zaburi 52 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Hukumu ya Mungu 1-2 Kwa mukubwa wa waimbaji. Mashairi ya Daudi yanayoelekea wakati Doegi wa Edomu alipomwendea Saulo na kumujulisha kwamba Daudi amemwendea Ahimeleki. 3 Mbona, ewe jitu, unajivunia mabaya unayotendea waaminifu. 4 Kila wakati unawaza maangamizi. Ulimi wako ni kama wembe mukali. Unafikiria tu kutenda mabaya. 5 Wewe unapenda ubaya kuliko uzuri, unapenda uongo kuliko ukweli. 6 Ewe mudanganyifu mukubwa, unapenda mambo ya kuangamiza wengine. 7 Kwa hiyo Mungu atakuangamiza milele, atakunyanyua na kukuondoa katika nyumba yako; atakuongoa katika inchi ya wenye kuishi. 8 Watu wa haki wataona, wataogopa, na kisha watakuchekelea na kusema: 9 “Muangalie yaliyomupata mutu huyu! Yeye hakutaka Mungu akuwe kimbilio lake, lakini alitegemea wingi wa mali yake, na kutafuta humo usalama wake!” 10 Lakini mimi ni kama muzeituni mubichi, unaostawi katika nyumba ya Mungu. Ninategemea wema wake milele na milele. 11 Ee Mungu, nitakushukuru siku zote, kwa ajili ya mambo uliyofanya. Nitatangaza kwamba wewe ni muzuri, mbele ya watu wako waaminifu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo