Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 51 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kuomba usamehe

1-2 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi inayoelekea wakati nabii Natani alipomufikia kwa kumwonya juu ya uzinzi alioufanya na Batiseba.

3 Unihurumie, ee Mungu, kadiri ya wema wako; uyafute makosa yangu, kadiri ya wingi wa rehema yako.

4 Unisafishe kabisa kosa langu; unitakase zambi yangu.

5 Ninaitikia kabisa makosa yangu, siku zote ninaona waziwazi zambi yangu.

6 Nimekukosea wewe peke yako, nimetenda mabaya mbele yako. Hivi uamuzi wako ni wa haki, hukumu yako haipotoki.

7 Mimi ni mukosaji tangia kuzaliwa kwangu, mwenye zambi tangia tumbo la mama yangu.

8 Wewe unataka moyo wa ukweli; hivyo unifundishe kuwa na moyo wa hekima.

9 Unitakase kwa hisopo, nikuwe safi, unisafishe, nikuwe mweupe pee.

10 Unijaze furaha na shangwe, unifurahishe tena, mimi ambaye uliniponda.

11 Ugeuke, usiangalie zambi zangu; uyafute makosa yangu yote.

12 Ee Mungu, uniumbie moyo safi, uweke ndani yangu roho mupya na inayoimarika.

13 Usinitupe mbali nawe; usiondoe roho yako takatifu ndani yangu.

14 Unirudishie furaha ya wokovu wako, uniimarishe kwa Roho wako mwema.

15 Halafu nitawafundisha wakosaji njia zako, nao wenye zambi watarudi kwako.

16 Uniokoe kutoka kosa la kumwanga damu, ee Mungu, Mungu mwokozi wangu, nami nitaimba kwa sauti kwamba umeniokoa.

17 Ee Bwana, uniwezeshe kusema, midomo yangu itangaze sifa zako.

18 Kweli wewe haupendezwi na sadaka. Hautaki nikutolee sadaka za kuteketezwa.

19 Sadaka ninayokutolea, ee Mungu, ni roho munyenyekevu. Haukatai moyo munyenyekevu na wa kutubu.

20 Ee Mungu, upendezwe na kuutendea mazuri Sayuni; uzijenge tena upya kuta za Yerusalema.

21 Halafu utapendezwa na sadaka za haki: ndizo sadaka za kuteketezwa na za kuteketezwa nzima. Ngombe dume watatolewa juu ya mazabahu yako.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan