Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 49 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Upumbafu wa kutegemea mali

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora.

2 Musikie jambo hili, enyi watu wote! Mutege masikio, enyi wakaaji wote wa dunia.

3 Musikilize wote, wakubwa na wadogo, enyi watajiri na wakosefu.

4 Maneno yangu ni mazitomazito; mawazo yangu ni ya hekima.

5 Ninatega sikio, nisikilize mezali, ninafafanua kitendawili kwa muziki wa zeze.

6 Kwa nini niogope wakati wa hatari, wakati ninapozungukwa na uovu wa waadui?

7 Watu waovu wanategemea mali zao, wanajisifia wingi wa utajiri wao.

8 Lakini mwanadamu hawezi hata kidogo kujikomboa mwenyewe; hawezi kumulipa Mungu bei ya maisha yake,

9 maana malipo ya ukombozi wa maisha ni kubwa sana. Hawezi kutoa kitu chochote kinachotosha,

10 kimwezeshe aendelee kuishi siku zote, bila kuona kaburi.

11 Inaonekana wazi kuwa hata wenye hekima wanakufa, nao wapumbafu na wajinga vilevile. Wote wanawaachia wengine mali zao.

12 Ingawa walisema kwamba udongo ni wao, lakini ni makaburi ndiyo nyumba zao hata milele, ni makao yao vizazi hata vizazi.

13 Mwanadamu hadumu katika utajiri wake; anakufa tu kama nyama.

14 Hayo ndiyo yanayowapata wanaojitumainia kwa upumbafu, ndio mwisho wa wale wanaojivunia mali zao.

15 Wanaongozwa kama kondoo mpaka katika kuzimu; kifo ndiye muchungaji wao. Wanashuka moja kwa moja katika kaburi. Miili yao inaozea huko. Kuzimu inakuwa makao yao.

16 Lakini Mungu atanikomboa kutoka katika kuzimu, ataniopoa kutoka huko.

17 Usihangaike ukiona mutu anatajirika, wala mali yake ikiongezeka zaidi na zaidi.

18 Maana atakapokufa hatachukua kitu chochote, mali yake haitashuka huko chini pamoja naye.

19 Hata akijitukuza katika maisha haya, na kusifiwa kwa sababu ya kufanikiwa,

20 atakwenda kukutana na babu zake waliomutangulia kufa, ambao hawawezi kuona tena mwangaza.

21 Mwanadamu hadumu katika utajiri wake: anakufa tu kama nyama.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan