Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 48 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Sayuni, muji wa Mungu

1 Zaburi ya Wakora.

2 Yawe, ni mukubwa; anastahili kusifiwa sana katika muji wake, ndio mulima wake mutakatifu.

3 Sayuni, mulima wa Mungu, unapendeza kwa urefu; muji wa Mufalme mukubwa ni furaha ya ulimwengu.

4 Mungu analinda pango zake za kukimbilia; yeye anajulikana kuwa upango wake.

5 Wafalme walikusanyika, wakaenda pamoja kushambulia.

6 Lakini walipouona Sayuni, wakashangaa; wakashikwa na hofu na kukimbia.

7 Hofu kubwa iliwashika, wakasikia uchungu kama mama anayezaa,

8 kama vile wenye kurushwa na upepo mukali wa mashariki, ambao unavunjavunja mashua kubwa sana za Tarsisi.

9 Yote tuliyosikia tumejionea wenyewe katika muji wa Yawe wa majeshi, katika muji wa Mungu wetu: Mungu atauimarisha milele.

10 Ee Mungu, tunakumbuka wema wako tunapokuwa katika hekalu lako.

11 Jina lako linasifiwa kila pahali, sifa zako zinaenea fasi zote katika dunia. Kwa mukono wako umetenda kwa haki.

12 Watu wa Sayuni wafurahi! Watu wa Yuda washangilie, kwa sababu ya hukumu yako ya haki!

13 Mutembee huko Sayuni, muuzunguke, muihesabu minara yake.

14 Muangalie kuta zake na kuchunguza pango zake za kukimbilia, mupate kuelezea vizazi vitakavyokuja kwamba:

15 “Huyu ni Mungu, Mungu wetu milele! Atakuwa mwongozi wetu milele!”

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan