Zaburi 46 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mungu yuko upande wetu 1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora: Kwa mutindo wa Sauti ya juu kabisa. 2 Mungu ni kimbilio letu na nguvu yetu; yeye ni musaada wetu wakati wa taabu. 3 Kwa hiyo hatutaogopa kitu chochote, hata dunia ikiyeyuka na milima kutikisika kutoka bahari, 4 hata kama bahari ikichafuka na kutisha, na milima ikitetemeka kwa machafuko yake. 5 Kuna muto ambao maji yake yanafurahisha muji wa Mungu, makao matakatifu ya Mungu Mukubwa. 6 Mungu yuko katika muji huo, nao hauwezi kutikiswa; Mungu ataupatia musaada kila asubui. 7 Mataifa yanakasirika na falme zinatikisika; Mungu ananguruma, nayo dunia inayeyuka. 8 Yawe wa majeshi yuko pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu. 9 Mukuje muone matendo ya Yawe. Muone maajabu aliyofanya katika dunia. 10 Anakomesha vita popote katika dunia. Anavunjavunja pinde na mikuki, nayo magari ya vita anayateketeza. 11 Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu! Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote; mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!” 12 Yawe wa majeshi yuko pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo