Zaburi 45 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mashairi ya kumusifu mufalme 1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo: “Mayungiyungi.” Mashairi ya Wakora. Wimbo wa mapenzi. 2 Moyo wangu umejaa mawazo mazuri: ninamutungia mufalme mashairi yangu, ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi hodari. 3 Wewe ni muzuri kuliko wanadamu wote, maneno yako ni rehema tupu, Mungu amekubariki milele. 4 Ujifungie upanga wako, ewe shujaa! Wewe ni mutukufu na mwenye mamlaka. 5 Songa mbele kwa utukufu upate ushindi, utetee ukweli na kulinda haki. Mukono wako utende mambo makubwa. 6 Mishale yako ni mikali, inapenya mioyo ya waadui za mufalme; nayo mataifa yanaanguka chini yako. 7 Kiti chako cha kifalme ni imara, kinadumu milele kama cha Mungu. Wewe unatawala watu wako kwa haki. 8 Unapenda haki na kuchukia uovu. Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupendelea kuliko wenzako; amekuweka kuwa mufalme kwa kukupakaa mafuta ya kufurahisha. 9 Nguo zako zinanuka marasi, udi, na mudalasini; muziki wa vinubi unakufurahisha katika nyumba ya pembe za tembo. 10 Wabinti za wafalme ni kati ya wanaokupokea, naye malkia amesimama kwa kuume kwako, amevaa mapambo ya zahabu safi kabisa ya Ofiri. 11 Sikiliza binti, ufikiri! Tega sikio lako: sahau sasa taifa lako na jamaa yako. 12 Uzuri wako unavuta moyo wa mufalme; yeye ni bwana yako, lazima umutii. 13 Watu wa Tiro watakuletea zawadi; watajiri watajipendekeza kwako. 14 Binti wa mufalme anaingia, naye ni muzuri kabisa! Nguo yake imefumwa na nyuzi za zahabu. 15 Akiwa amevaa nguo za rangi nyingi, anaongozwa kwa mufalme, akisindikizwa na wabinti wenzake. 16 Kwa furaha na shangwe wanafika huko, na kuingia katika nyumba ya mufalme. 17 Ee mufalme, utapata watoto wengi watakaotawala pahali pa babu zako; utawafanya watawale katika dunia yote. 18 Nitalifanya jina lako litukuzwe katika vizazi vyote, nayo mataifa yatakusifu milele. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo