Zaburi 43 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maombi ya mukimbizi yanaendelea 1 Unipatie haki yangu, ee Mungu; uyatetee maneno yangu mbele ya watu wabaya; uniokoe na watu waongo na waovu. 2 Ninakimbilia kwako, ee Mungu; kwa nini umenitupilia mbali? Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza kwa kuteswa na adui yangu? 3 Utumie mwangaza na ukweli wako viniongoze, vinipeleke kwenye mulima wako mutakatifu, kwenye makao yako. 4 Hapo, ee Mungu, nitakwenda kwenye mazabahu yako; nitakuja kwako, ee Mungu, wewe furaha yangu kubwa. Nitakusifu kwa zeze, ee Mungu, Mungu wangu. 5 Mbona ninahuzunika hivyo katika moyo? Kwa nini ninahangaika hivyo ndani mwangu? Nitamutumainia Mungu, nitamusifu tena yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo