Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 43 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maombi ya mukimbizi yanaendelea

1 Unipatie haki yangu, ee Mungu; uyatetee maneno yangu mbele ya watu wabaya; uniokoe na watu waongo na waovu.

2 Ninakimbilia kwako, ee Mungu; kwa nini umenitupilia mbali? Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza kwa kuteswa na adui yangu?

3 Utumie mwangaza na ukweli wako viniongoze, vinipeleke kwenye mulima wako mutakatifu, kwenye makao yako.

4 Hapo, ee Mungu, nitakwenda kwenye mazabahu yako; nitakuja kwako, ee Mungu, wewe furaha yangu kubwa. Nitakusifu kwa zeze, ee Mungu, Mungu wangu.

5 Mbona ninahuzunika hivyo katika moyo? Kwa nini ninahangaika hivyo ndani mwangu? Nitamutumainia Mungu, nitamusifu tena yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan