Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 42 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


SEHEMU YA PILI (Zaburi 42–72 ) Maombi ya mukimbizi

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Mashairi ya Wakora.

2 Kama pongo anavyotamani maji ya kijito, ndivyo ninavyokutamani, ee Mungu wangu!

3 Ninasikia kiu ya Mungu, kiu ya Mungu Mwenye Uzima. Nitafika kwake wakati gani na kuuona uso wake?

4 Machozi ni chakula changu muchana na usiku; ninaambiwa kila siku: “Mungu wako yuko wapi?”

5 Katika huzuni yangu, ninakumbuka jinsi nilivyokwenda na kundi la watu na kuwaongoza kwenda katika nyumba ya Mungu wakipiga vigelegele vya shukrani, kundi la watu likifanya sherehe!

6 Mbona ninaugua hivyo katika moyo? Kwa nini ninahangaika hivyo ndani yangu? Nitamutumainia Mungu, maana nitamusifu tena yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.

7 Roho yangu imeregea kabisa, kwa hiyo ninakukumbuka wewe, ee Mungu, kutoka katika eneo la Yordani, kutoka mulima Hermoni na Mizari.

8 Mafuriko juu ya mafuriko yananguruma, mawimbi na zoruba yako vinanifunika.

9 Yawe atanijalia wema wake muchana; nami nitamwimbia wimbo wa sifa usiku, nitamwomba Mungu anayenipa uzima.

10 Ninamwambia Mungu, yeye kikingio changu: “Kwa nini umenisahau? Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza kwa kuteswa na adui yangu?”

11 Nimepondekana kwa ajili ya matukano yao, wanaponiuliza kila siku: “Mungu wako, yupo wapi?”

12 Mbona ninaugua hivyo katika moyo? Kwa nini ninahangaika hivyo ndani yangu? Nitamutumainia Mungu, maana nitamusifu tena Mungu, anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan