Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mashairi ya sifa

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.

2 Nilimungojea Yawe kwa uvumilivu, akanielekea na kusikia kilio changu.

3 Aliniondoa katika shimo la hatari, alinitoa katika matope mengi, akanisimamisha salama juu ya mulima, na kuziimarisha hatua zangu.

4 Alinifundisha wimbo mupya, wimbo wa sifa kwa Mungu wetu. Wengi wataona, wataogopa, na kisha watamutumainia Yawe.

5 Heri mutu anayemutumainia Yawe, mutu asiyejiunga na watu wenye majivuno, watu waliopotoka kwa kuabudu miungu ya uongo.

6 Ee Yawe, Mungu wangu, umetufanyia maajabu mengi, na mipango yako juu yetu haihesabiki; hakuna yeyote anayekuwa kama wewe. Kama ningeweza kusimulia hayo yote, hesabu yake ingenishinda.

7 Wewe hautaki sadaka za kuteketezwa kwa moto wala matoleo, sadaka za nyama za kuteketezwa wala za kusamehewa zambi, lakini umenipa masikio nikusikie.

8 Halafu nikasema: “Ninakuja. Katika kitabu imeandikwa juu yangu.

9 Ninataka kutimiza mapenzi yako, ee Mungu wangu; sheria yako ninaishika kwa moyo wangu wote!”

10 Nimesimulia habari njema ya ukombozi, mbele ya kusanyiko kubwa la watu. Kama unavyojua, ee Yawe, mimi sikujizuia kuitangaza.

11 Sikuficha katika moyo wangu ukombozi ulionijalia. Nimetangaza siku zote kwamba wewe ni mwokozi mwaminifu. Sikuficha kusanyiko kubwa la watu wema wako na uaminifu wako.


Kuomba musaada

12 Ee Yawe, usikose kunirehemu! Wema na uaminifu wako vinilinde.

13 Hatari zisizohesabika zinanizunguka, maovu yangu yananisonga hata siwezi kuona; ni mengi kuliko nywele zangu, nami nimevunjika moyo.

14 Upendezwe, ee Yawe, kuniokoa; ee Yawe, ukuje haraka kunisaidia.

15 Wote wanaokusudia kuniangamiza, wafezeheke pamoja! Hao wanaotamani niumie, warudi nyuma na kuzarauliwa!

16 Hao wanaonisimanga, wafezeheke kwa kushindwa kwao!

17 Lakini wanaokutafuta wafurahi na kushangilia. Wanaopenda uwaokoe waseme siku zote: “Yawe ni mukubwa!”

18 Mimi ni masikini na mukosefu, ee Bwana; lakini wewe haukunisahau. Wewe ni musaada wangu na mwokozi wangu; ukuje, ee Mungu wangu, usikawie!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan