Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kuomba musaada

1 Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Zaburi ya Daudi.

2 Ee Mungu, muteteaji wa haki yangu, unijibu ninapoomba. Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia; unionee huruma na kusikia maombi yangu.

3 Ninyi watu, mpaka wakati gani mutachafua jina langu? Mpaka wakati gani mutapendelea mambo ya ovyo na kusema uongo?

4 Mujue kwamba Yawe amejichagulia mutu wake wa haki. Yawe anasikia kila mara ninapomwomba.

5 Mukasirike lakini musitende zambi. Mufikiri katika vitanda vyenu na kunyamaza.

6 Mutoe sadaka zinazokuwa sawa, na kumutumainia Yawe.

7 Wengi wanasema: “Heri tungefanikiwa tena! Ee Yawe, utuangalie kwa wema!”

8 Lakini mimi umenijalia furaha kubwa ndani ya moyo, kuliko ya hao wanaokuwa na divai na ngano kwa wingi.

9 Ninalala na kupata usingizi kwa amani; wewe peke yako, ee Yawe, unaniweka salama.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan