Zaburi 4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kuomba musaada 1 Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Zaburi ya Daudi. 2 Ee Mungu, muteteaji wa haki yangu, unijibu ninapoomba. Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia; unionee huruma na kusikia maombi yangu. 3 Ninyi watu, mpaka wakati gani mutachafua jina langu? Mpaka wakati gani mutapendelea mambo ya ovyo na kusema uongo? 4 Mujue kwamba Yawe amejichagulia mutu wake wa haki. Yawe anasikia kila mara ninapomwomba. 5 Mukasirike lakini musitende zambi. Mufikiri katika vitanda vyenu na kunyamaza. 6 Mutoe sadaka zinazokuwa sawa, na kumutumainia Yawe. 7 Wengi wanasema: “Heri tungefanikiwa tena! Ee Yawe, utuangalie kwa wema!” 8 Lakini mimi umenijalia furaha kubwa ndani ya moyo, kuliko ya hao wanaokuwa na divai na ngano kwa wingi. 9 Ninalala na kupata usingizi kwa amani; wewe peke yako, ee Yawe, unaniweka salama. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo