Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mwanadamu mbele ya Mungu

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa Yedutuni. Zaburi ya Daudi.

2 Nilisema: “Nitayachunga maisha yangu, kusudi nisitende zambi kwa usemi wangu. Nitafunga midomo yangu waovu wanapokuwa karibu nami.”

3 Nilikuwa kama bubu, bila kusema kitu, nilinyamaza lakini sikupata faida. Mateso yangu yalizidi kuwa makali,

4 mahangaiko yangu yakaniunguza katika moyo. Kadiri nilivyowaza ndivyo nilivyotaabika, kisha maneno haya yakanitoka:

5 “Ee Yawe, unijulishe mwisho wangu, siku zangu za kuishi zimenibakia ngapi, nijue namna maisha yangu yanavyopita upesi!”

6 Kumbe umenipimia maisha mafupi sana! Maisha yangu si kitu mbele yako. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!

7 Kweli, kila mutu anapita kama kivuli; masumbuko yake yote ni bure tu; anakusanya mali, hajui atakayeipata!

8 Na sasa, ee Bwana, ninatazamia nini? Tumaini langu ni kwako wewe!

9 Uniokoe katika makosa yangu yote; usikubali wapumbafu wanichekelee.

10 Niko kama bubu, sisemi kitu, kwa maana wewe ndiwe uliyetenda hayo.

11 Usiniazibu tena; ninamalizika kwa mapigo yako.

12 Unapomwazibu mutu zambi zake kwa kumwadibisha, unaharibu kama nondo kile anachokipenda. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!

13 Usikie maombi yangu, ee Yawe, usikilize kilio changu, usikae kimya ninapolia. Maana, mimi ni kama mugeni tu anayepita, ni musafiri kama vile babu zangu wote walivyokuwa.

14 Uache kuniangalia nipate kufurahi kidogo, mbele sijaaga dunia na kutoweka kabisa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan