Zaburi 36 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Uovu wa mwanadamu 1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi, mutumishi wa Yawe. 2 Zambi inaongea na mutu mwovu, ndani kabisa ya moyo wake; kuogopa Mungu si kitu kwake. 3 Mwovu anajipendelea mwenyewe, anafikiri uovu wake hautagunduliwa na kulaaniwa. 4 Kila anachosema ni uovu na uongo; ameacha kutumia hekima na kutenda mema. 5 Anapolala anawaza kutenda maovu, anajiweka katika njia isiyokuwa nzuri, wala hachukii uovu. Wema wa Mungu 6 Wema wako, ee Yawe, unaenea hata mbinguni; uaminifu wako unafika hata kwenye mawingu. 7 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama vilindi vya bahari. Wewe, ee Yawe, unawalinda wanadamu na nyama. 8 Kweli wema wako ni bora! Wanadamu wanakimbilia kwenye kivuli cha mabawa yako. 9 Unawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako; unawakunywesha katika muto wa wema wako. 10 Wewe ndiwe asili ya uzima; kwa mwangaza wako tunaona mwangaza. 11 Uendelee kuwatendea mema wale wanaokutambua; uzidi kuokoa wenye moyo wenye kunyooka. 12 Usikubali wenye majivuno wanishambulie, wala watu waovu wanikimbize. 13 Kumbe watenda maovu wameanguka; wameangushwa chini, hawawezi kuinuka. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo