Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 36 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Uovu wa mwanadamu

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi, mutumishi wa Yawe.

2 Zambi inaongea na mutu mwovu, ndani kabisa ya moyo wake; kuogopa Mungu si kitu kwake.

3 Mwovu anajipendelea mwenyewe, anafikiri uovu wake hautagunduliwa na kulaaniwa.

4 Kila anachosema ni uovu na uongo; ameacha kutumia hekima na kutenda mema.

5 Anapolala anawaza kutenda maovu, anajiweka katika njia isiyokuwa nzuri, wala hachukii uovu.


Wema wa Mungu

6 Wema wako, ee Yawe, unaenea hata mbinguni; uaminifu wako unafika hata kwenye mawingu.

7 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama vilindi vya bahari. Wewe, ee Yawe, unawalinda wanadamu na nyama.

8 Kweli wema wako ni bora! Wanadamu wanakimbilia kwenye kivuli cha mabawa yako.

9 Unawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako; unawakunywesha katika muto wa wema wako.

10 Wewe ndiwe asili ya uzima; kwa mwangaza wako tunaona mwangaza.

11 Uendelee kuwatendea mema wale wanaokutambua; uzidi kuokoa wenye moyo wenye kunyooka.

12 Usikubali wenye majivuno wanishambulie, wala watu waovu wanikimbize.

13 Kumbe watenda maovu wameanguka; wameangushwa chini, hawawezi kuinuka.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan