Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kuomba musaada

1 Zaburi ya Daudi. Uwapinge, ee Yawe, hao wanaonipinga; uwashambulie hao wanaonishambulia.

2 Utwae ngao yako na kikingio chako, uinuke ukuje kunisaidia!

3 Chukua mukuki na upanga wako kwa kuwazuia wale wanaonifuata. Uniambie mimi kwamba utaniokoa.

4 Wapate haya na kuzarauliwa, hao wanaotaka kupoteza maisha yangu! Warudishwe nyuma na kufezeheka, hao wanaonitafutia hasara.

5 Wakuwe kama maganda yanayopeperushwa na upepo, wakikimbizwa na malaika wa Yawe!

6 Njia yao ikuwe ya giza na utelezi, wakifukuzwa na malaika wa Yawe!

7 Maana walinitegea mitego bila sababu; walinichimbia shimo bila neno lolote.

8 Maangamizi yawapate wao kwa rafla, wanaswe katika mutego wao wenyewe, watumbukie katika shimo lao wenyewe!

9 Hivi nitamufurahia Yawe; nitashangilia kwa sababu yeye ameniokoa.

10 Nitamwambia Yawe kwa moyo wangu wote: “Wewe, ee Yawe, hakuna anayekuwa kama wewe! Wewe unawaokoa wamasikini kutoka makucha ya wenye nguvu, wamasikini na wakosefu kutoka mikono ya wanyanganyi.”

11 Washuhuda wakorofi wanajitokeza, wananiuliza mambo nisiyoyajua.

12 Wananilipa mabaya kwa mazuri; nami pekee nimebaki ukiwa.

13 Lakini wao walipokuwa wagonjwa, mimi nilivaa magunia kuonyesha huzuni, nilijitesa kwa kufunga kula chakula. Niliomba nikikuwa nimeinamisha kichwa.

14 Nikakuwa kama ninamulilia rafiki au ndugu yangu. Nilikwenda huku na huko kwa huzuni, kama mutu anayeomboleza kifo cha mama yake.

15 Lakini mimi nilipoanguka, walikusanyika kunisimanga. Walikusanyika kuniuzi. Wageni nisiowajua walinizomea bila kukoma, wala hakuna aliyewazuia.

16 Walinichekelea, walinisagia meno.

17 Ee Yawe, utaangalia tu mpaka wakati gani? Uniokoe kutoka mashambulio yao; uokoe maisha yangu kutoka simba wakali hao.

18 Hivi nitakushukuru kati ya kusanyiko kubwa la watu; nitakutukuza kati ya kundi kubwa la watu.

19 Usiwaache waadui hao wabaya wanisimange, hao wanaonichukia bure, wafurahie mateso yangu.

20 Hawasemi vizuri juu ya wengine, wanatunga tu uongo juu ya wanainchi watulivu.

21 Wananishitaki kwa sauti, wakisema: “Sawa! Sawa! Tumeona wenyewe uliyotenda!”

22 Lakini wewe Yawe unaona jambo hilo. Usinyamaze, ee Yawe, usikae mbali nami.

23 Uinuke, ee Yawe, unitetee; ukuje, ee Mungu wangu, uangalie maneno yangu.

24 Ee Yawe, Mungu wangu, unitetee, unitendee kulingana na haki yako. Usiwaache waadui zangu wanisimange.

25 Usiwaache waseme: “Tumefanikiwa sawa tulivyotaka!” au waseme: “Tumemumaliza huyu!”

26 Uwaache hao wanaofurahia hasara yangu, washindwe wote na kufezeheka. Hao wote wanaojiona bora kuliko mimi, wapate haya na kufezeheka.

27 Lakini wanaotaka kuona kwamba sina kosa, wakuwe na furaha tele, waseme siku zote: “Yawe ni mukubwa! Anapendezwa na kumupatia mutumishi wake uheri.”

28 Hivi nitatangaza haki yako; nitasema sifa zako muchana kutwa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan