Zaburi 34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Sifa kwa ajili ya wema wa Mungu 1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi alipojifanya mwenda-wazimu mbele ya mufalme Abimeleki naye akamufukuza na Daudi akajiendea. 2 Nitamutukuza Yawe nyakati zote, sitaacha hata kidogo kutaja sifa zake. 3 Mimi nitajisifu kwa ajili ya Yawe; wanyenyekevu wasikie na kufurahi. 4 Mumutukuze Yawe pamoja nami, wote pamoja tulisifu jina lake. 5 Nilimwomba Yawe, naye akanijibu, na kuniondoa katika hofu zangu zote. 6 Mumugeukie Mungu mupate kufurahi; nanyi hamutafezeheka hata kidogo. 7 Masikini alimulilia Yawe, naye akamusikia, na kumwokoa katika taabu zake zote. 8 Malaika wa Yawe anawalinda wote wanaomwabudu, na kuwaokoa kutoka katika hatari. 9 Mupime muone jinsi Yawe ni muzuri. Heri mutu anayekimbilia kwake. 10 Mumwabudu Yawe, enyi watakatifu wake, maana wenye kumwabudu hawakosewi kitu. 11 Hata simba wakali wanakosewa na kusikia njaa, lakini wanaomutafuta Yawe hawakosewi chochote kizuri. 12 Mukuje, enyi vijana munisikilize, nami nitawafundisha kumwabudu Yawe. 13 Unatamani kufurahia maisha, kuishi maisha marefu na kufurahia mazuri? 14 Basi, uache kusema mabaya, na kuepuka kusema uongo. 15 Ujiepushe na uovu, utende mazuri; utafute amani na kuifuatilia. 16 Yawe anawaangalia watu wa haki, na kusikiliza malalamiko yao; 17 lakini anawapinga watu wanaotenda maovu, kusudi afute majina yao kutoka katika dunia. 18 Watu wa haki wakimulilia Yawe, yeye anawasikia, na kuwaokoa katika taabu zao zote. 19 Yawe ni karibu na wenye kuvunjika moyo; anawaokoa wote waliokata tamaa kabisa. 20 Mateso ya mutu wa haki ni mengi, lakini Yawe anamwokoa kutoka katika yote. 21 Analinda viungo vya mwili wake wote, hakuna hata mufupa wake mumoja utakaovunjwa. 22 Ubaya unawaletea waovu kifo; wanaowachukia watu wa haki wataazibiwa. 23 Yawe anaokoa maisha ya watumishi wake, wote wanaomukimbilia hawataazibiwa. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo