Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mashairi ya kumusifu Mungu

1 Mushangilie kwa sababu ya Yawe, enyi watu wa haki! Watu wa usawa ndio wanaostahili kumusifu Mungu.

2 Mumusifu Yawe kwa zeze; mumwimbie kwa kinubi cha nyuzi kumi.

3 Mumwimbie wimbo mupya; mupige kinubi vizuri na kushangilia.

4 Neno la Yawe ni la usawa; na matendo yake yote ni ya kuaminika.

5 Yawe anapenda haki na sheria. Dunia imejaa wema wake.

6 Mbingu ziliumbwa kwa neno la Yawe, na vyote vinavyokuwa ndani yake kwa pumzi ya kinywa chake.

7 Alikusanya maji ya bahari kama katika chupa, akavifunga vilindi vya bahari ndani ya gala.

8 Dunia yote imwogope Yawe! Wakaaji wote wa dunia wamwabudu!

9 Maana alisema, na ulimwengu ukakuwa; alitoa amri, nao ukajitokeza.

10 Yawe anavunja mipango ya mataifa, na anabadilisha mawazo yao.

11 Mipango ya Yawe inadumu milele; kusudi lake linadumu kwa vizazi vyote.

12 Heri taifa ambalo Mungu wake ni Yawe; heri wale aliowachagua kuwa watu wake mwenyewe!

13 Yawe anaangalia chini kutoka mbinguni, na kuwaona wanadamu wote.

14 Kutoka kwenye kiti chake cha kifalme, anawaangalia wakaaji wote wa dunia.

15 Yeye anaunda mioyo ya watu wote, yeye anajua kila kitu wanachofanya.

16 Mufalme hawezi kuokolewa kwa kuwa na kundi kubwa; wala shujaa hapati ushindi kwa nguvu zake kubwa.

17 Farasi wa vita hafai kitu kwa kupata ushindi; nguvu zake nyingi haziwezi kumwokoa mutu.

18 Yawe anawaangalia wale wanaomwabudu, watu ambao wanatumainia wema wake.

19 Yeye anawaokoa katika kifo, anawalinda wakati wa njaa.

20 Mioyo yetu inamutumainia Yawe. Yeye ni musaidizi wetu na ngao yetu.

21 Tunafurahi kwa sababu yake; tunatumainia jina lake takatifu.

22 Wema wako ukae nasi, ee Yawe, kwa maana tumekuwekea tumaini letu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan