Zaburi 32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maondoleo ya zambi 1 Zaburi ya Daudi: Mashairi. Heri mutu aliyesamehewa kosa lake, mutu ambaye zambi yake imeondolewa kabisa. 2 Heri mutu ambaye Yawe hamuhesabii kosa, mutu ambaye hana udanganyifu ndani ya moyo wake. 3 Nilipokuwa sijaitikia zambi yangu, nilikuwa muzaifu sana kwa kulia muchana kutwa. 4 Muchana na usiku mukono wako ulinilemea; nguvu zangu zikakwisha, kama maji yanavyokauka wakati wa kipwa. 5 Kisha niliitikia makosa yangu mbele yako, wala sikuficha uovu wangu. Nilisema kwamba nitaungama makosa yangu mbele ya Yawe. Nawe ukanisamehe zambi yangu. 6 Kwa hiyo, kila mwaminifu akutolee maombi wakati wa taabu. Mafuriko ya maji hayatamufikia. 7 Wewe unanificha kwa kunilinda wakati wa taabu. Ninazungukwa na ukombozi wako. 8 Mungu anasema: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayofuata. Nitakushauria kwa uangalifu mukubwa. 9 Usikuwe mupumbafu kama farasi au nyumbu, ambao lazima wafungwe kamba ndani ya kinywa, kama sivyo hawatakukaribia.” 10 Watu waovu watapata mateso mengi, lakini wanaomutumainia Yawe wanazungukwa na wema wake. 11 Mufurahi na kushangilia kwa sababu ya Yawe, enyi watu wa haki; mupige vigelegele vya shangwe, enyi wenye moyo wa usawa. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo