Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maombi ya shukrani

1 Mashairi yanayoelekea muzinduo wa hekalu. Zaburi ya Daudi.

2 Ninakutukuza, ee Yawe, maana umeniokoa, wala haukuwaacha waadui zangu wanisimange.

3 Ee Yawe, Mungu wangu, nilikulilia, nawe ukaniponyesha.

4 Ee Yawe, umeniokoa kutoka kuzimu; umenipa tena uzima, umenitoa kutoka kati ya wafu.

5 Mumwimbie Yawe sifa, enyi waaminifu wake; mukumbuke utakatifu wake na kumushukuru.

6 Hasira yake inadumu muda kidogo tu, upendo wake unadumu milele. Kilio kinaweza kuwa usiku, lakini muchana kunatokea furaha.

7 Mimi nilipofanikiwa, nilisema: “Sitashindwa hata kidogo!

8 Kwa upendo wako, ee Yawe, umeniimarisha kama mulima mukubwa.” Lakini ukajificha mbali nami, nami nikafazaika.

9 Nilikulilia wewe, ee Yawe; nilikusihi, ee Yawe:

10 “Utapata faida gani nikikufa na kushuka mpaka katika shimo la wafu? Mavumbi ya wafu yanaweza kukusifu? Yanaweza kusimulia uaminifu wako?

11 Usikie, ee Yawe, unihurumie; ee Yawe, unisaidie!”

12 Wewe umegeuza malalamiko yangu kuwa ngoma ya furaha; umeniondolea huzuni yangu, ukanijaza furaha.

13 Mimi nitakusifu wala sitakaa kimya. Ee Yawe, Mungu wangu, nitakushukuru milele.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan