Zaburi 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kuomba musaada Furaha ya kweli 1 Zaburi ya Daudi. Inaelekea wakati alipomukimbia mwana wake Abusaloma. 2 Ee Yawe, angalia ginsi waadui zangu wanavyokuwa wengi. Ni wengi sana hao wanaonishambulia. 3 Wengi wanasema juu yangu: “Hautapata musaada wowote kwa Mungu.” 4 Lakini wewe, ee Yawe, unanizunguka kama ngao; kwako ninapata utukufu na ushindi. 5 Ninakulilia kwa sauti, ee Mungu, nawe unanisikiliza kutoka kwenye mulima wako mutakatifu. 6 Ninalala na kupata usingizi, ninaamuka tena, maana wewe ni tegemeo langu. 7 Sitaogopa maelfu ya watu wanaonizunguka kila upande. 8 Ee Yawe, ee Mungu wangu, wewe unayevunja waadui zangu wote mataya, unayeponda waovu meno, simama sasa uniokoe! 9 Yawe ndiwe unayeokoa; uwape baraka watu wako. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo