Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kuomba musaada

1 Zaburi ya Daudi. Ninakulilia, ee Yawe! Ewe kikingio changu, usikuwe kama kiziwi kwangu. Usikuwe kama haunisikilizi, nisikuwe kama wale wanaoshuka katika shimo la wafu.

2 Sikiliza sauti ya ombi langu, ninapokulilia unisaidie, ninapoinua mikono yangu kuelekea hekalu lako takatifu.

3 Usiniazibu pamoja na watu wabaya, wale watenda maovu wanaosema vizuri na wenzao, kumbe wanajaa ubaya ndani ya moyo.

4 Uwalipe kwa kadiri ya matendo yao, kufuatana na maovu waliyotenda. Uwalipe kwa kadiri ya matendo yao wenyewe; uwatendee yale wanayostahili.

5 Hawashuguliki na matendo ya Yawe; hawatambui mambo aliyofanya. Kwa sababu hiyo atawabomoa, wala hatawajenga tena upya.

6 Atukuzwe Yawe, maana amesikiliza ombi langu.

7 Yawe ndiye nguvu na ngao yangu; tegemeo la moyo wangu ni kwake. Amenisaidia, nami nikashangilia kwa moyo wote; kwa wimbo wangu ninamushukuru.

8 Yawe ni nguvu ya watu wake; yeye ni kimbilio la mufalme aliyemuchagua.

9 Ee Mungu, uwaokoe watu wako; uwabariki watu hao wanaokuwa mali yako. Ukuwe muchungaji wao na kuwalinda milele.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan