Zaburi 24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mufalme Mukubwa 1 Zaburi ya Daudi. Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Yawe; ulimwengu na wote wanaoishi ndani yake ni mali yake. 2 Maana yeye aliweka misingi ya dunia juu ya bahari; aliisimika imara juu ya maji mengi. 3 Nani atakayepanda kwa mulima wa Yawe? Nani atakayekaa katika hekalu lake takatifu? 4 Ni mutu wa matendo mema na moyo safi, asiyefuata mambo ya ovyo, wala kuapa kwa uongo. 5 Mutu huyo atapokea baraka kwa Yawe, na haki yake kwa Mungu mwokozi wake. 6 Ndiyo hali ya kizazi cha watu wanaomutafuta yeye, watu wanaomutafuta Mungu wa Yakobo. 7 Mufunguke, enyi milango; mufunguke, enyi milango ya tangia zamani, kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie. 8 Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu? Ni Yawe, mwenye nguvu na uwezo; Yawe, mwenye uwezo katika vita. 9 Mufunguke, enyi milango, mufunguke, enyi milango ya tangia zamani, kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie. 10 Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu? Ni Yawe, wa majeshi, yeye ndiye Mufalme mwenye utukufu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo