Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mufalme Mukubwa

1 Zaburi ya Daudi. Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Yawe; ulimwengu na wote wanaoishi ndani yake ni mali yake.

2 Maana yeye aliweka misingi ya dunia juu ya bahari; aliisimika imara juu ya maji mengi.

3 Nani atakayepanda kwa mulima wa Yawe? Nani atakayekaa katika hekalu lake takatifu?

4 Ni mutu wa matendo mema na moyo safi, asiyefuata mambo ya ovyo, wala kuapa kwa uongo.

5 Mutu huyo atapokea baraka kwa Yawe, na haki yake kwa Mungu mwokozi wake.

6 Ndiyo hali ya kizazi cha watu wanaomutafuta yeye, watu wanaomutafuta Mungu wa Yakobo.

7 Mufunguke, enyi milango; mufunguke, enyi milango ya tangia zamani, kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie.

8 Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu? Ni Yawe, mwenye nguvu na uwezo; Yawe, mwenye uwezo katika vita.

9 Mufunguke, enyi milango, mufunguke, enyi milango ya tangia zamani, kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie.

10 Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu? Ni Yawe, wa majeshi, yeye ndiye Mufalme mwenye utukufu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan