Zaburi 20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kuomba ushindi 1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. 2 Yawe akujibu unapokuwa katika taabu; jina la Mungu wa Yakobo likulinde. 3 Akupelekee musaada kutoka katika hekalu lake; akukinge tokea kwenye mulima Sayuni. 4 Akumbuke sadaka zako zote; akubali sadaka zako za kuteketezwa. 5 Akujalie unayotamani ndani ya moyo wako, afanikishe mipango yako yote. 6 Tutashangilia kwa ajili ya ushindi wako; tutainua bendera kwa kutukuza jina la Mungu wetu. Yawe akutimizie mapenzi yako yote! 7 Ninajua Yawe atamusaidia mufalme aliyemuchagua, atamujibu tokea pahali pake patakatifu mbinguni; kwa mukono wake wenye nguvu atamujalia ushindi mukubwa. 8 Wamoja wanajivunia magari ya vita, wengine farasi wao. Lakini sisi tunajivunia Yawe, Mungu wetu. 9 Hao wanajikwaa na kuanguka; lakini sisi tunasimama na kuimarika. 10 Ee Yawe, umujalie mufalme ushindi, utujibu wakati tunapokuomba. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo