Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mufalme muchaguliwa wa Mungu

1 Kwa nini mataifa yanafanya fujo? Mbona watu wanafanya shauri la bure?

2 Wafalme wa dunia wanajitayarisha, watawala wanashauriana pamoja kumwasi Yawe na muchaguliwa wake.

3 Wanasema: “Tujiondoe katika utawala wao; tutupilie mbali minyororo yao!”

4 Yule anayetawala juu mbinguni anawachekelea na kuwazarau.

5 Kisha, anawakaripia kwa kasirani na kuwatisha kwa hasira, akisema:

6 “Nimemusimika mufalme niliyemuchagua; anatawala Sayuni, mulima wangu mutakatifu!”

7 Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.

8 Uniombe nami nitakupa mataifa kuwa urizi wako, na dunia nzima kuwa mali yako.

9 Utawaponda kwa fimbo ya chuma, utawavunja kama chungu cha mufinyanzi!’ ”

10 Sasa, enyi wafalme, mutumie akili; musikilize onyo hili, enyi watawala wa dunia.

11-12 Mumutumikie Yawe kwa woga; muiname mbele ya mwana wake na kutetemeka, kusudi asikasirike, nanyi musiangamie kwa rafla; kwa maana hasira yake inawaka haraka. Heri wote wanaokimbilia kwake!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan