Zaburi 2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mufalme muchaguliwa wa Mungu 1 Kwa nini mataifa yanafanya fujo? Mbona watu wanafanya shauri la bure? 2 Wafalme wa dunia wanajitayarisha, watawala wanashauriana pamoja kumwasi Yawe na muchaguliwa wake. 3 Wanasema: “Tujiondoe katika utawala wao; tutupilie mbali minyororo yao!” 4 Yule anayetawala juu mbinguni anawachekelea na kuwazarau. 5 Kisha, anawakaripia kwa kasirani na kuwatisha kwa hasira, akisema: 6 “Nimemusimika mufalme niliyemuchagua; anatawala Sayuni, mulima wangu mutakatifu!” 7 Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako. 8 Uniombe nami nitakupa mataifa kuwa urizi wako, na dunia nzima kuwa mali yako. 9 Utawaponda kwa fimbo ya chuma, utawavunja kama chungu cha mufinyanzi!’ ” 10 Sasa, enyi wafalme, mutumie akili; musikilize onyo hili, enyi watawala wa dunia. 11-12 Mumutumikie Yawe kwa woga; muiname mbele ya mwana wake na kutetemeka, kusudi asikasirike, nanyi musiangamie kwa rafla; kwa maana hasira yake inawaka haraka. Heri wote wanaokimbilia kwake! |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo