Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Utukufu wa Mungu katika viumbe

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.

2 Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu; anga linaeleza kazi ya mikono yake.

3 Muchana unaupasha habari muchana unaofuata, usiku unaufahamisha usiku unaofuata.

4 Si kwa musemo au kwa maneno; wala hakuna sauti inayosikilika;

5 hata hivyo, ujumbe wao unaenea katika dunia yote, na habari zao zinafika miisho ya ulimwengu. Mungu amewekea jua makao yake katika anga;

6 nalo linatoka kama vile bwana-arusi kutoka chumba chake, linakimbia kwa furaha katika njia yake kama shujaa.

7 Linatokea kwa upande mumoja, na kuzunguka mpaka upande mwingine; hakuna kinachoweza kuepuka joto lake.


Sheria ya Mungu

8 Sheria ya Yawe ni kamilifu; inamupa mutu uzima mupya. Maagizo ya Yawe ni ya kuaminiwa; yanawapa wajinga hekima.

9 Kanuni za Yawe ni sawa; zinafurahisha moyo. Amri za Yawe ni safi; zinamufungua mutu macho.

10 Kumutii Yawe ni jambo jema; kunadumu milele. Maagizo ya Yawe ni sawa, yote ni ya haki kabisa.

11 Yanatamanika kuliko zahabu, kuliko zahabu safi kabisa. Ni matamu kuliko asali, kuliko asali safi kabisa.

12 Yananifundisha mimi mutumishi wako; kuyafuata kunaniletea zawadi kubwa.

13 Lakini nani anayeona makosa yake mwenyewe? Ee Mungu, unisamehe makosa nisiyoyajua.

14 Unikinge mimi mutumishi wako na makosa ya makusudi, usikubali hayo yanitawale. Hapo nitakuwa mukamilifu, wala sitakuwa na kosa kubwa.

15 Maneno ya kinywa changu, na mawazo ya moyo wangu, yakubalike mbele yako, ee Yawe, kikingio changu na mwokozi wangu!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan