Zaburi 15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Rafiki ya Mungu 1 Zaburi ya Daudi. Ee Yawe, nani atakayekaa katika hema yako? Nani atakayeishi juu ya mulima wako mutakatifu? 2-5 Ni mutu anayefanya hivi: anaishi katika ukamilifu, anatenda kwa haki siku zote, anasema ukweli kutoka ndani ya moyo, hatetani, hatendei rafiki yake uovu, hamutukani jirani yake, anazarau wapotevu, anaheshimu wanaomwabudu Yawe, hageuzi kiapo chake hata kikimuletea hasara, hakopeshi feza yake kwa kupata faida, wala kupokea kituliro kumutesa asiyekuwa na kosa. Mutu anayefanya vile, hatatikisika hata kidogo. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo