Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 143 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kuomba musaada

1 Zaburi ya Daudi. Usikie maombi yangu, ee Yawe! Ulitegee ombi langu sikio, maana wewe ni mwaminifu; unijibu kwa sababu ya haki yako.

2 Usinitie katika hukumu mimi mutumishi wako, maana hakuna yeyote anayekuwa mwenye haki mbele yako.

3 Waadui zangu wamenifuatilia, wameniangusha chini kabisa, wameniikalisha katika giza kama mutu aliyekufa zamani.

4 Roho yangu imeregea kabisa; moyo wangu unaugua.

5 Ninakumbuka siku za zamani, ninafikiri juu ya yote uliyotenda, ninawazawaza matendo yako.

6 Ninakunyooshea mikono yangu. Ninakuhitaji wewe, kama inchi kavu inavyohitaji mvua.

7 Ee Yawe, unijibu haraka; maana roho yangu imeregea kabisa! Usinigeuzie mugongo, kusudi nisikuwe kama wale wanaoshuka katika shimo la wafu.

8 Kila asubui unionyeshe wema wako, maana ninakutumainia. Unifundishe mwenendo wa kufuata, maana ninakutolea moyo wangu.

9 Uniokoe, ee Yawe, kutoka waadui zangu, maana ninakimbilia kwako.

10 Unifundishe kutimiza mapenzi yako, maana wewe ni Mungu wangu! Roho wako muzuri aniongoze katika njia sawa.

11 Ulinde uzima wangu, ee Yawe, kwa ajili ya jina lako, uniondoe katika taabu, kwa ajili ya haki yako.

12 Kwa ajili ya wema wako uwakomeshe waadui zangu, uwaangamize wote wanaonitesa, maana mimi ni mutumishi wako.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan