Zaburi 142 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maombi ya mutu aliyeachwa pekee 1 Mashairi ya Daudi alipokuwa ndani ya pango. 2 Ninamulilia Yawe kwa sauti kubwa, ninamusihi Yawe kwa sauti kubwa. 3 Ninamutolea malalamiko yangu, ninamwelezea taabu zangu. 4 Roho yangu inaporegea kabisa, yeye yuko, anajua mwenendo wangu. Waadui wamenitegea mitego katika njia ninayopita. 5 Nikiangalia kwa kuume kwangu na kungojea, ninaona hakuna mutu wa kunisaidia; sina tena nafasi ya kukimbilia, hakuna mutu anayenijali. 6 Ninakulilia wewe, ee Yawe! Wewe ni kimbilio langu; wewe ni hitaji langu lote katika inchi ya wenye uzima. 7 Usikilize kilio changu, maana nimetabanika sana; uniokoe kutoka watesaji wangu, maana wamenizidi nguvu. 8 Uniondoe humu katika kifungo, kusudi nipate kukushukuru, nikijiunga na watu wa haki kwa sababu ya vyote ulivyonitendea. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo