Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 141 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Hatari za tamaa mbaya

1 Kwa mukubwa wa waimbaji: Zaburi ya Daudi. Ninakulilia, ee Yawe, ukuje haraka kunisaidia! Usikilize sauti yangu wakati ninapokuita!

2 Upokee maombi yangu kama ubani; ninapoinua mikono yangu kwako, unikubali kama sadaka ya magaribi.

3 Ee Yawe, ulinde kinywa changu, uweke mulinzi kwenye mulango wa kinywa changu.

4 Unikinge nisielekee kufanya mabaya, nisijishugulishe na matendo maovu, nisijiunge na watu wanaotenda mabaya, wala nisishiriki hata kidogo katika karamu zao.

5 Afazali mutu mwema anipige kwa kunionya; lakini sikubali hata kidogo kusifiwa na wabaya, maana ninaomba siku zote juu ya maovu yao.

6 Wakubwa wao watakapopondwa juu ya mawe, ndipo watatambua kwamba maneno yangu yalikuwa mazuri.

7 Mifupa yao itatawanywa kwenye midomo ya kuzimu kama kuni zilizopasuliwa vipandevipande!

8 Lakini mimi ninakutegemea, ee Yawe, Mungu wangu; ninakimbilia kwako, usiniache katika hatari.

9 Unikinge na mitego waliyonitegea, uniepushe na wavu wa hao watu waovu.

10 Waovu wanaswe katika mitego yao wenyewe, wakati mimi ninaponyoka.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan