Zaburi 14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Uovu wa watu (Ang. Zab 53 ) 1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo: “Hakuna Mungu.” Wote wamepotoka kabisa, matendo yao ni ya kuchukiza; hakuna hata mumoja anayetenda mazuri! 2 Yawe anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni aone kama kuna yeyote mwenye akili, kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu. 3 Lakini wote wamekosa, wote wamepotoka pamoja; hakuna anayetenda mazuri, hakuna hata mumoja. 4 Hao wanaotenda maovu hawajui kitu? Wanatafuna watu wangu kama mikate, wala hawajali Yawe. 5 Hapo watashikwa na hofu, maana Mungu ni pamoja na watu wa haki. 6 Unaweza kuvuruga mipango ya masikini, lakini Yawe ndiye kimbilio lake. 7 Heri ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Sayuni! Yawe atakapotengeneza hali ya watu wake, wazao wa Yakobo watashangilia; watu wa Israeli watafurahi. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo