Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Uovu wa watu
(Ang. Zab 53 )

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo: “Hakuna Mungu.” Wote wamepotoka kabisa, matendo yao ni ya kuchukiza; hakuna hata mumoja anayetenda mazuri!

2 Yawe anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni aone kama kuna yeyote mwenye akili, kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu.

3 Lakini wote wamekosa, wote wamepotoka pamoja; hakuna anayetenda mazuri, hakuna hata mumoja.

4 Hao wanaotenda maovu hawajui kitu? Wanatafuna watu wangu kama mikate, wala hawajali Yawe.

5 Hapo watashikwa na hofu, maana Mungu ni pamoja na watu wa haki.

6 Unaweza kuvuruga mipango ya masikini, lakini Yawe ndiye kimbilio lake.

7 Heri ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Sayuni! Yawe atakapotengeneza hali ya watu wake, wazao wa Yakobo watashangilia; watu wa Israeli watafurahi.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan