Zaburi 137 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maombolezo katika inchi ya kigeni 1 kandokando ya mito ya Babeli tuliikaa tukilia, tulipokumbuka Sayuni. 2 Katika miti ya inchi ile, tulitundika zeze zetu. 3 Waliotupeleka kuwa watumwa walitaka tuwaimbie; watesaji wetu walitaka tuwafurahishe, wakituambia: “Mutuimbie nyimbo zimoja za Sayuni!” 4 Namna gani tunaweza kuimba wimbo wa Yawe katika inchi ya kigeni? 5 Ee Yerusalema, kama nikikusahau, mukono wangu wa kuume ukauke! 6 Ulimi wangu ukuwe muzito, kama nisipokukumbuka wewe, ee Yerusalema, nisipokufurahia kuliko furaha yangu kubwa! 7 Ee Yawe, usisahau mambo Waedomu waliyotenda, siku ile Yerusalema iliponyanganywa; kumbuka maneno haya waliyosema: “Mubomoe Yerusalema! Muongoe hata na misingi yake!” 8 Ee Babeli, muharibifu wee! Heri yule atakayekulipiza mabaya uliyotutendea! 9 Heri yule atakayetwaa watoto wako na kuwapondaponda juu ya jiwe! |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo