Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 135 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Sifa kwa Mungu

1 Haleluia! Musifu jina la Yawe, mumusifu, enyi watumishi wake.

2 Mumusifu, enyi munaokaa katika nyumba yake, ndani ya viwanja vya nyumba ya Mungu wetu!

3 Mumusifu Yawe kwa sababu yeye ni muzuri; mumutukuze kwa nyimbo, maana inafaa.

4 Yawe amemuchagua Yakobo kuwa wake, watu wa Israeli kuwa mali yake mwenyewe.

5 Ninajua hakika kwamba Yawe ni mukubwa; Bwana wetu ni mukubwa kupita miungu yote.

6 Yawe anafanya chochote anachotaka, mbinguni, katika dunia, ndani ya bahari na shimo ndefu.

7 Analeta mawingu kutoka miisho ya dunia, anapiga umeme na kunyesha mvua, anavumisha upepo kutoka gala zake.

8 Aliwaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, wazaliwa wa watu na wa nyama vilevile.

9 Alifanya miujiza na maajabu kwako, ee Misri, mufalme wa Misri na wakubwa wake wote.

10 Aliangamiza mataifa mengi, akawaua wafalme wenye nguvu

11 kama vile Sihoni mufalme wa Waamori, Ogi mufalme wa Basani, na wafalme wote wa Kanana.

12 Alikamata inchi zao kuwa urizi wa watu wake; zikuwe urizi wa watu wake Israeli.

13 Jina lako, ee Yawe, linadumu milele, utakumbukwa nyakati zote.

14 Yawe atawatetea watu wake; na kuwaonea huruma watumishi wake.

15 Miungu ya uongo ya mataifa ni feza na zahabu, imetengenezwa kwa mikono ya wanadamu.

16 Ina vinywa, lakini haisemi; ina macho, lakini haioni.

17 Ina masikio, lakini haisikii; wala haiwezi hata kuvuta pumzi.

18 Wote walioifanya wafanane nayo, kila mumoja anayeitegemea!

19 Enyi watu wa Israeli, mumutukuze Yawe! Enyi makuhani, mumutukuze Yawe!

20 Enyi Walawi, mumutukuze Yawe! Enyi munaomwabudu Yawe, mumutukuze!

21 Atukuzwe Yawe katika Sayuni, atukuzwe katika makao yake Yerusalema. Haleluia!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan