Zaburi 130 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kuomba musaada 1 Wimbo wa safari za kidini. Tokea humu katika taabu inayonilemea, ninakulilia, ee Yawe. 2 Ee Bwana, usikie sauti yangu, ulitegee ombi langu sikio. 3 Ee Yawe, kama ungekumbuka maovu yetu, nani, ee Bwana wetu, angeweza kuishi? 4 Lakini kwako tunapata usamehe, kusudi sisi tukuheshimu. 5 Ninamutumainia Yawe kwa moyo wangu wote. Ninaaminia sana neno lake. 6 Ninamungojea Yawe kuliko vile wazamu wanavyongojea mapambazuko, ndiyo, kuliko vile wazamu wanavyongojea mapambazuko. 7 Ee Israeli, umutumainie Yawe, maana Yawe ni mwenye wema, naye ana nguvu kubwa ya kutukomboa. 8 Yeye atawakomboa watu wa Israeli kutoka katika maovu yao yote. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo