Zaburi 129 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maombi juu ya waadui za Israeli 1 Wimbo wa safari za kidini. Kila mutu katika Israeli aseme: “Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu”. 2 Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu, lakini hawakunishinda. 3 Walinikata vidonda katika mugongo, kama wanavyolima matuta katika shamba. 4 Lakini Yawe ni mwenye haki; ametutosha katika utumwa wa hao waovu. 5 Wafezeheke na kurudishwa nyuma, wote wale wanaouchukia Sayuni. 6 Wakuwe kama nyasi juu ya paa la nyumba, ambazo zinanyauka mbele ya kukomaa, 7 anayezikata hajazi kitanga cha mukono, wala anayezikusanya haenezi fungu. 8 Naye anayepita karibu asiwaambie: “Yawe awabariki! Tunawabariki kwa jina la Yawe!” |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo