Zaburi 128 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Baraka ya wenye kumutii Mungu 1 Wimbo wa safari za kidini. Heri wote wanaomwabudu Yawe, wanaoishi kufuatana na amri zake. 2 Utapata matunda ya jasho lako, utafurahi na kupata uheri. 3 Muke wako atakuwa kama muzabibu wenye matunda mengi; watoto wako kama vichipukizi vya muzeituni kuzunguka meza yako. 4 Kweli, hivi ndivyo atakavyobarikiwa mutu anayemwabudu Yawe. 5 Yawe akubariki kutokea Sayuni! Uone uheri wa Yerusalema, siku zote za maisha yako. 6 Uishi na hata uwaone wajukuu wako! Amani ikuwe na Israeli! |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo