Zaburi 127 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Bila Mungu kazi ya mwanadamu haifai kitu 1 Wimbo wa safari za kidini: wa Solomono. Yawe asipoijenga nyumba, wanaoijenga wanajisumbua bure. Yawe asipoulinda muji, wanaoulinda wanakesha bure. 2 Munajisumbua bure kuamuka asubui mapema na kuchelewa kwenda kupumzika magaribi, mujipatie chakula kwa jasho lenu. Mungu anatimiza mahitaji ya wapendwa wake hata wanapolala. 3 Watoto ni urizi kutoka kwa Yawe; uzao ni zawadi yake kwetu sisi. 4 Watoto wanaokuwa na nguvu, ni kama mishale katika mikono ya askari. 5 Heri mutu anayekuwa na mishale hiyo kwa wingi. Hatashindwa atakaposamba na waadui zake kwenye tribinali. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo