Zaburi 124 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mungu ni mulinzi wetu 1 Wimbo wa safari za kidini. Ninyi wote munaokuwa katika Israeli museme: “Kama Yawe asingalikuwa upande wetu”. 2 “Kama Yawe asingalikuwa upande wetu, wakati ule tuliposhambuliwa na waadui, 3 hakika tungalimezwa tukikuwa wazima, wakati hasira yao ilipowaka juu yetu. 4 Tungalichukuliwa na maji mengi, tungalifunikwa na muto. 5 Tungalizamishwa na maporomoko ya maji!” 6 Yawe atukuzwe! Hakutuachilia katika meno yao. 7 Tumeponyoka kama ndege katika mutego; mutego umefyatuka, nasi tukaponyoka. 8 Musaada wetu unatoka kwa Yawe, aliyeumba mbingu na dunia. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo