Zaburi 123 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kuomba huruma 1 Wimbo wa safari za kidini. Ninainua macho kwako, ee Yawe, wewe unayeikaa huko juu mbinguni! 2 Kama watumishi wanavyomutegemea bwana wao, kama mujakazi anavyomutegemea bibi mukubwa wake, ndivyo nasi tunavyokutegemea wewe, ee Yawe, Mungu wetu, mpaka hapo utakapotuonea huruma. 3 Utuhurumie, ee Yawe, utuhurumie, maana tumezarauliwa kupita kipimo. 4 Tumeshiba muda murefu mazarau ya watajiri, nayo masimango ya wenye kiburi. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo