Zaburi 122 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Sifa za Yerusalema 1 Wimbo wa Safari za kidini. Wa Daudi. Nilifurahi waliponiambia: “Twende kwenye nyumba ya Yawe.” 2 Sasa tuko tumesimama kwenye milango yako, ee Yerusalema! 3 Yerusalema ni muji uliojengwa kusudi makundi ya watu yakutane humo. 4 Humo ndimo makabila yanamofika, ndiyo, makabila ya Yawe, kwa kumushukuru Yawe kama Waisraeli walivyoagiza. 5 Humo kulikuwa viti vya kifalme kwa kuamua maneno, ndivyo viti vya ukoo wa Daudi. 6 Muuombee Yerusalema amani mukisema: “Wote wanaokupenda wakae katika amani! 7 Ndani ya kuta zinazokuzunguka kuwe amani, nao usalama ukuwe ndani ya nyumba zako nzuri!” 8 Kwa ajili ya jamaa na wandugu zangu, ee Yerusalema, ninakutakia amani! 9 Kwa ajili ya nyumba ya Yawe, Mungu wetu, ninakuombea upate uheri! |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo