Zaburi 121 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mungu ni mulinzi wetu 1 Wimbo wa safari za kidini. Ninainua macho kwenye milima. Musaada wangu unatoka wapi? 2 Musaada wangu unatoka kwa Yawe, aliyeumba mbingu na dunia. 3 Hatakuacha uanguke; mulinzi wako hasinzii. 4 Kweli mulinzi wa Israeli hasinzii wala halali. 5 Yawe ni mulinzi wako; yuko upande wako wa kuume kwa kukukinga. 6 Muchana jua halitakuchoma, wala mwezi hautakuzuru usiku. 7 Yawe atakukinga na uovu wote; atayalinda salama maisha yako. 8 Yawe atakulinda katika shuguli zako zote tangu sasa na hata milele. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo