Zaburi 12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kuomba musaada 1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa vyombo vyenye nyuzi nane. Zaburi ya Daudi. 2 Unisaidie, ee Yawe! Watu wema wamekwisha; waaminifu wametoweka kati ya watu. 3 Kila mumoja anamudanganya mwenzake; anabembeleza lakini ni kwa moyo wa unafiki. 4 Ee Yawe, ukomeshe midomo hiyo ya kudanganya, na ndimi hizo zinazojigamba. 5 Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?” 6 Lakini Yawe anasema: “Kwa sababu wamasikini wanaugua, na wakosefu wanalia, sasa ninasimama, nami nitawapa usalama wanaoutazamia.” 7 Ahadi za Yawe ni safi, safi kama feza iliyosafishwa katika chungu, kama feza iliyosafishwa mara saba. 8 Utulinde, ee Yawe, utukinge siku zote na kizazi hiki kiovu. 9 Waovu wanazunguka popote; upotovu unatukuzwa kati ya watu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo