Zaburi 118 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maombi ya shukrani 1 Mumushukuru Yawe, kwa sababu ni muzuri! Wema wake unadumu milele! 2 Watu wa Israeli waseme: “Wema wake unadumu milele.” 3 Wazao wa Haruni waseme: “Wema wake unadumu milele.” 4 Wote wanaomwabudu Yawe waseme: “Wema wake unadumu milele.” 5 Katika taabu yangu nilimwomba Yawe, naye akanisikia na kuniweka huru. 6 Yawe yuko nami, siogopi kitu; mwanadamu ataweza kunifanya nini? 7 Yawe yuko nami kwa kunisaidia; nami nitawaona waadui zangu wameshindwa. 8 Afazali kumukimbilia Yawe kuliko kumutumainia mwanadamu. 9 Afazali kumukimbilia Yawe, kuliko kuwatumainia waongozi wa dunia. 10 Mataifa yote yalinizunguka, lakini kwa jina la Yawe nikayaangamiza! 11 Yalinizunguka kila upande, lakini kwa jina la Yawe, nikayaangamiza! 12 Yalinizunguka, mengi kama nyuki, lakini yakateketea kama kichaka ndani ya moto; kwa jina la Yawe niliyaangamiza! 13 Nilishambuliwa sana karibu nishindwe, lakini Yawe alinisaidia. 14 Yawe ni nguvu yangu kubwa; yeye mwenyewe ndiye wokovu wangu. 15 Sauti za furaha ya ushindi zikasikilika katika hema za watu wa haki: “Mukono wa Yawe umetenda mambo makubwa! 16 Mukono wa nguvu wa Yawe umeleta ushindi! Mukono wa Yawe umetenda mambo makubwa!” 17 Sitakufa. Nitaishi na kueleza matendo ya Yawe. 18 Yawe ameniazibu sana, lakini hakuniachilia nikufe. 19 Munifungulie milango ya watu wa haki, niingie na kumushukuru Yawe! 20 Huu ndio mulango wa Yawe, watu wa haki watapitia humo. 21 Ninakushukuru, ee Yawe, kwa kunijibu; kwa sababu wewe ni wokovu wangu. 22 Jiwe lililokataliwa na wajengaji, limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi. 23 Ni Yawe aliyefanya jambo hili, nalo ni ajabu sana kwetu. 24 Hii ndiyo siku aliyoifanya Yawe; tushangilie na kufurahi. 25 Tafazali utuokoe, ee Yawe! Tafazali utubariki, ee Yawe! 26 Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Yawe! Tunawabariki kutoka katika nyumba ya Yawe. 27 Yawe ni Mungu; yeye ametujalia mwangaza wake. Mushike matawi katika mikono, mukiandamana mpaka kwenye mazabahu. 28 Wewe ni Mungu wangu, ninakushukuru; ninakutukuza, ee Mungu wangu. 29 Mumushukuru Yawe kwa sababu ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo