Zaburi 113 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Sifa kwa Mungu mwenye utukufu 1 Haleluia! Enyi watumishi wa Yawe, musifu jina lake! 2 Jina lake litukuzwe, sasa na hata milele. 3 Kutoka mashariki na hata magaribi, litukuzwe jina la Yawe! 4 Yawe anatawala juu ya mataifa yote, utukufu wake unafika juu ya mbingu. 5 Nani anayekuwa kama Yawe, Mungu wetu? Yeye anakaa juu kabisa; 6 lakini anachungulia chini, aangalie mbingu na dunia. 7 Anamwinua muzaifu toka katika mavumbi, anamunyanyua mukosefu toka yalala, 8 na kumuweka pamoja na wakubwa, pamoja na wakubwa wa watu wake. 9 Anamurudishia heshima mwanamuke anayekuwa tasa; anamufurahisha kwa kumujalia watoto. Haleluia! |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo