Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 112 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Furaha ya mutu mwema

1 Haleluia! Heri mutu anayemuheshimu Yawe, anayefurahia sana kushika amri zake.

2 Wazao wake watakuwa wenye nguvu katika inchi; watoto wa watu wa usawa watapata baraka.

3 Ndani ya nyumba yake kutakuwa mali nyingi; haki yake utadumu milele.

4 Mutu wa usawa anaangaziwa mwangaza katika giza; yeye ni mwenye huruma, rehema, na haki.

5 Mutu muzuri anakopesha bila faida; anafanya shuguli zake kwa kutumia haki.

6 Hatashindwa hata kidogo; atakumbukwa milele.

7 Haogopi habari mbaya; moyo wake unasimama imara na anamutegemea Yawe.

8 Yuko imara ndani ya moyo, wala hataogopa; naye ataona waadui zake wakishindwa.

9 Anatoa kwa moyo safi, anawapa wamasikini. Haki yake inadumu milele. Ana nguvu na sifa.

10 Watu waovu wanaona hayo na kuuzika. Wanasaga meno kwa chuki na kutoweka. Matumaini ya mutu mubaya yanapotea bure.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan