Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 110 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kusimikwa kwa mufalme muchaguliwa

1 Zaburi ya Daudi. Yawe anamwambia bwana wangu: “Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”

2 Yawe ataeneza mamlaka yako kutoka Sayuni; utatawala juu ya waadui zako wote.

3 Watu wako watajitolea, siku utakapokwenda kuwapiga waadui. Juu ya milima mitakatifu vijana wako watakufikia, kama umande unaotokeza asubui mapema.

4 Yawe amekuapia hivi wala hatabadilisha nia yake: “Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.”

5 Bwana wetu yuko karibu nawe; atawaponda wafalme atakapokasirika.

6 Atayahukumu mataifa na kuwaua watu wengi; atawaponda waongozi kila nafasi katika dunia.

7 Mufalme atakunywa maji ya kijito katika njia, kisha atainua kichwa kwa ushindi.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan