Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 109 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Malalamiko ya mutu anayekuwa katika taabu

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Wimbo wa Daudi. Usinyamaze, ee Mungu, ninayekusifu!

2 Watu waovu na wadanganyifu wananishambulia, wanasema uongo juu yangu.

3 Wanasema maovu juu yangu, na kunishambulia bila sababu.

4 Ingawa niliwapenda, walinishitaki. Hata hivyo, niliwaombea.

5 Wananilipa mabaya kwa mazuri yangu, na chuki kwa mapendo yangu.

6 Umuweke mwamuzi mubaya juu ya adui yangu; na anayemushitaki amupeleke mbele ya baraza.

7 Anapohukumiwa apatikane na kosa; malalamiko yake yahesabiwe kuwa kosa lingine.

8 Siku za maisha yake zikuwe chache, mutu mwingine akamate kazi yake!

9 Watoto wake wakuwe wayatima, na muke wake akuwe mujane!

10 Watoto wake watangetange na kuombaomba; wafukuzwe katika mabaki ya nyumba zao!

11 Anayemudai kitu amunyanganye mali yake yote, na wageni wakule mapato ya jasho lake!

12 Kusikuwe mutu wa kumutendea mema, au kuwatunza watoto wake wayatima!

13 Wazao wake wote wakufe; jina lake lisahauliwe katika kizazi kinachokuja!

14 Yawe akumbuke uovu wa babu zake, zambi za mama yake zisifutwe hata kidogo!

15 Yawe akumbuke zambi zao siku zote; lakini wao wenyewe wasahauliwe katika dunia.

16 Mwovu huyo hajali kabisa kutenda mema, lakini anatesa wamasikini, wakosefu, na wenye moyo wenye kuvunjika mpaka kufa.

17 Yeye alipenda kulaani watu; laana imupate yeye mwenyewe. Hakuwatakia wengine baraka; basi, asipate baraka yeye mwenyewe.

18 Kwake kulaani ni kama kuvaa nguo; basi, laana hizo zimulowanishe kama maji, zimwingie katika mifupa yake kama mafuta.

19 Laana zimufunike kama nguo, zimuzunguke siku zote kama mukaba.

20 Yawe awalipe hayo hao watu wanaonishitaki, hao wanaosema mabaya juu yangu.

21 Lakini, ee Yawe, Bwana wangu, unitendee kwa heshima ya jina lako. Wema wako ni muzuri. Basi, uniokoe!

22 Mimi ni masikini na mukosefu; ninaumizwa mpaka ndani ya moyo wangu.

23 Ninatoweka kama kivuli cha magaribi; nimepeperushwa kama nzige.

24 Magoti yangu yanaregea kwa ajili ya kufunga kula chakula; nimebaki mifupa na ngozi.

25 Watu wananichekelea; wanaponiona wanatikisa vichwa vyao kwa kunizarau.

26 Unisaidie, ee Yawe, Mungu wangu; uniokoe kufuatana na wema wako.

27 Uwaonyeshe watu kuwa wewe ndiwe uliyetenda hayo. Wewe, ee Yawe, ndiwe uliyefanya hivyo.

28 Uwaache walaani, lakini wewe unibariki; wanaonishambulia wafezeheke, nami mutumishi wako nifurahi.

29 Waadui zangu wazungukwe na mazarau; wajifunike haya yao kama vile nguo.

30 Nitamushukuru sana Yawe kwa sauti; nitamusifu kati ya kundi kubwa la watu,

31 kwa maana yeye anamutetea mukosefu, kwa kumwokoa kutoka kwa wale wanaomuhukumu kufa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan