Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 105 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mungu na watu wake
( 1 Sik 16.8-22 )

1 Mumushukuru Yawe, mutangaze ukubwa wake, mujulishe mataifa mambo aliyotenda!

2 Mushangilie, mumwimbie Mungu sifa, mueleze matendo yake ya ajabu!

3 Mujisifu kwa ajili ya jina lake takatifu; wanaomutafuta Yawe wafurahi.

4 Mumutafute Yawe mwenye nguvu; mumutafute Yawe siku zote.

5 Mukumbuke matendo ya ajabu aliyotenda, miujiza yake na hukumu alizotoa,

6 enyi wazao wa Abrahamu mutumishi wake, enyi wazao wa Yakobo muchaguliwa wake.

7 Yeye ndiye Yawe, Mungu wetu; hukumu zake zina nguvu katika dunia yote.

8 Yeye anashika agano lake milele, anatimiza ahadi zake kwa vizazi elfu.

9 Anashika agano alilofanya na Abrahamu, na ahadi aliyomwapia Isaka.

10 Alimusimamishia Yakobo ahadi yake, akamuhakikishia agano hilo la milele.

11 Alisema: “Nitawapa inchi ya Kanana, nayo itakuwa mali yenu wenyewe.”

12 Watu wa Mungu walikuwa wachache tu, tena walikuwa wageni katika inchi ya Kanana.

13 Walitangatanga kutoka taifa mpaka taifa, kutoka inchi moja mpaka inchi ingine.

14 Lakini Mungu hakuruhusu wateswe; kwa ajili yao aliwaonya wafalme, akisema:

15 “Musiwaguse wachaguliwa wangu; musiwazuru manabii wangu!”

16 Mungu alileta njaa katika inchi yao, akafunga njia zao zote za kupata chakula.

17 Lakini aliwatangulizia mutu mumoja, Yosefu aliyekuwa ameuzishwa kuwa mutumwa.

18 Walimufunga miguu kwa minyororo, na kikomo cha chuma kwenye shingo,

19 mpaka kile alichotabiri kilipotimia. Neno la Yawe likahakikisha kwamba alikuwa na haki.

20 Mufalme wa Misri akaamuru afunguliwe; mutawala wa mataifa akamwachilia huru.

21 Alimuweka kuwa musimamizi wa serikali yake, na mukubwa wa mali yake yote,

22 awaongoze wakubwa wa serikali yake sawa anavyopenda, na kuwafundisha wazee wake hekima.

23 Halafu Israeli akaingia katika inchi ya Misri; Yakobo akakuwa mugeni katika inchi ya Hamu.

24 Yawe akawafanya watu wake wazae sana; akawajalia nguvu kuliko waadui zao.

25 Aliwafanya Wamisri wawachukie watu wake, wakawatendea watumishi wake vibaya.

26 Kisha akamutuma Musa mutumishi wake, akamutuma pamoja na Haruni muchaguliwa wake.

27 Wakafanya maajabu ya Mungu kati ya Wamisri, na miujiza katika inchi hiyo ya Hamu.

28 Mungu akaleta giza juu ya inchi; lakini Wamisri wakakataa kutii amri zake.

29 Akageuza mito yao kuwa damu, akaua samaki wao wote.

30 Vyura wakajaa juu ya inchi yao, hata katika nyumba ya mufalme.

31 Mungu akaamuru, kukatokea makundi ya mainzi, na imbu katika inchi yote.

32 Kwa pahali pa mvua akawatumia mvua ya mawe, na radi iliyounguza inchi yao yote;

33 akaharibu mizabibu na miti yao ya tini; akavunja miti ya inchi yao.

34 Mungu akaamuru, kukatokea nzige, na mapanzi maelfu yasiyohesabiwa;

35 wakatafuna mimea yote katika inchi, wakakula mazao yao yote.

36 Aliua wazaliwa wa kwanza katika inchi yao, ndilo chipukizi la kwanza la jamaa za Wamisri.

37 Kisha akawaondoa watu wa Israeli katika inchi, wakikuwa na feza na zahabu; wala hakuna hata mumoja wao aliyejikwaa.

38 Wamisri walifurahia kuondoka kwao, maana hofu iliwashika kwa sababu yao.

39 Mungu alitandaza wingu juu ya watu wake, na moto kusudi uwaangazie usiku.

40 Waliomba, naye akawaletea kwale, akawapa mukate kutoka mbinguni kwa wingi.

41 Alipasua jiwe maji yakabubujika; yakatiririka katika jangwa kama muto.

42 Alikumbuka ahadi yake takatifu aliyomupa Abrahamu mutumishi wake.

43 Basi akawaondoa watu wake katika inchi, wachaguliwa wake wakaimba na kushangilia.

44 Aliwapa inchi za mataifa na kuwatolea mashamba ya wenyeji,

45 kusudi watu wake watii masharti yake, na kufuata sheria zake. Haleluia!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan