Zaburi 101 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mwenendo muzuri wa mufalme 1 Zaburi ya Daudi. Wimbo wangu unaelekea wema na haki; ninauimba kwa heshima yako, ee Yawe. 2 Nitashikamana na mwenendo mukamilifu. Utakuja kwangu wakati gani? Nitaishi kwa ukamilifu ndani ya nyumba yangu; 3 sitavumilia hata kidogo mambo ya upuuzi. Ninachukia matendo ya watu wapotovu, mimi sitaambatana nayo. 4 Upotovu wowote ukuwe mbali nami; sitahusika kabisa na uovu. 5 Nitateketeza yule anayemuteta mwenzake, sitamuvumilia mwenye majivuno na kiburi. 6 Nitawaangalia waaminifu katika inchi, wapate kuishi pamoja nami. Watu wakamilifu, ndio watakaonitumikia. 7 Mwongo yeyote hatakaa ndani ya nyumba yangu; hakuna musema uongo atakayekaa kwangu. 8 Siku kwa siku nitawaangamiza waovu wote katika inchi; nitawaangamiza wabaya wote katika muji wa Yawe. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo