Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maombi juu ya mateso

1 Ee Yawe, mbona unasimama mbali? Kwa nini unajificha wakati tuko katika taabu?

2 Waovu wanatesa wamasikini kwa kiburi. Mitego yao iwanase wao wenyewe!

3 Mwovu anajisifia tamaa zake mbaya, anapata faida kwa njia mbaya, anazarau na kumukataa Yawe.

4 Katika majivuno yake anasema: “Mungu hatagundua. Hakuna Mungu.” Hayo ndiyo mawazo yake yote.

5 Njia za mwovu zinafanikiwa siku zote; hukumu zako ziko mbali na mawazo yake, na anazarau waadui zake wote.

6 Anawaza ndani ya moyo: “Sitakuwa na wasiwasi; sitapatwa na taabu katika maisha.”

7 Kinywa chake kimejaa laana, udanganyifu na ukorofi; ni mwepesi kusema maneno ya kuchukiza na maovu.

8 Anajificha karibu na vijiji akivizia, amwue kwa siri mutu asiyekuwa na kosa. Yuko macho kumuvizia muzaifu;

9 anajificha katika maficho yake kama simba. Anavizia apate kuwakamata wamasikini; anawanasa kwa mutego wake na kuwachukua.

10 Muzaifu anashambuliwa na kuangushwa chini; anaangushwa kwa ukali wa mutu mwovu.

11 Mwovu anawaza ndani ya moyo wake: “Mungu amesahau; ameficha uso wake, haoni kitu!”

12 Ee Yawe, simama sasa uwaazibu! Usiwasahau wanaoteswa.

13 Ee Mungu, kwa nini mwovu anakuzarau, na kusema kwamba wewe haujali kitu?

14 Lakini wewe unawaona wenye taabu na shida; nawe uko tayari kuwasaidia siku zote. Muzaifu anakutegemea wewe, ee Mungu, wewe umekuwa siku zote musaada wa yatima.

15 Uvunje nguvu za mutu mwovu; ukomeshe uovu wake wote, usikuwe tena.

16 Yawe ni mufalme milele na milele! Mataifa yatatoweka katika inchi yake.

17 Ee Yawe, unapokea maombi ya muzaifu; unamutia moyo na kumutegea sikio.

18 Utawatendea haki wayatima na wanaoteswa, mwanadamu anayekuwa mavumbi asiweze tena kuleta hofu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan