Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


SEHEMU YA KWANZA (Zaburi 1–41 )

1 Heri mutu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi, wala kukusanyika na wenye kuzarau;

2 lakini anafurahia sheria ya Yawe, na kuifikiri muchana na usiku.

3 Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya vijito, unaozaa matunda kwa wakati wake, na majani yake hayanyauki hata kidogo. Anafanikiwa katika yote anayofanya.

4 Lakini waovu si vile hata kidogo. Wao ni kama maganda yanayopeperushwa na upepo.

5 Kwa hiyo watu waovu wataanguka wakati wa hukumu, wenye zambi hawatashiriki katika kusanyiko la watu wa haki.

6 Maana Yawe anashugulikia njia ya watu wa haki; lakini njia ya waovu itaangamia.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan