Zaburi 1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002SEHEMU YA KWANZA (Zaburi 1–41 ) 1 Heri mutu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi, wala kukusanyika na wenye kuzarau; 2 lakini anafurahia sheria ya Yawe, na kuifikiri muchana na usiku. 3 Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya vijito, unaozaa matunda kwa wakati wake, na majani yake hayanyauki hata kidogo. Anafanikiwa katika yote anayofanya. 4 Lakini waovu si vile hata kidogo. Wao ni kama maganda yanayopeperushwa na upepo. 5 Kwa hiyo watu waovu wataanguka wakati wa hukumu, wenye zambi hawatashiriki katika kusanyiko la watu wa haki. 6 Maana Yawe anashugulikia njia ya watu wa haki; lakini njia ya waovu itaangamia. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo