Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Yoshua 16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Inchi ya Efuraimu na ya Manase

1 Sehemu wazao wa Yosefu waliyogawanyiwa kwa kura ilianzia karibu na muto Yordani, upande wa mashariki wa chemichemi ya Yeriko, na kupitia katika jangwa, hata kwenye sehemu za milima mpaka Beteli.

2 Kutoka Beteli, mupaka ulielekea Luzi ukapita Ataroti ambako Waarki waliishi.

3 Kisha ukashuka upande wa magaribi katika inchi ya Wayefeleti hata Beti-Horoni ya Chini na Gezeri na kuishia kwenye bahari ya Mediteranea.

4 Wazao wa Yosefu, ni kusema kabila la Manase na kabila la Efuraimu, walipewa inchi hiyo kuwa urizi wao.


Inchi ya kabila la Efuraimu

5 Watu wa kabila la Efuraimu kulingana na jamaa zao walipata sehemu yao ambayo mupaka wake upande wa mashariki ulipita Ataroti-Adari hata Beti-Horoni ya Juu,

6 na kuishia bahari ya Mediteranea. Kwa upande wa kaskazini mupaka ulipita Mikimetati na kwa mashariki yake ulizunguka na kuelekea Tanati-Shilo ambako ulipita upande wa mashariki hata Yanoa.

7 Kutoka Yanoa ulikwenda hata Ataroti na Nara, hata kufika Yeriko, ambako uliishia katika muto Yordani.

8 Kutoka Tapua, mupaka ulikwenda upande wa magaribi hata kijito cha Kana na kuishia bahari ya Mediteranea. Hii ndiyo inchi watu wa kabila la Efuraimu waliyopewa kulingana na jamaa zao,

9 pamoja na miji na vijiji ambavyo waliongezewa kutoka kwenye inchi ya kabila la Manase.

10 Waefuraimu hawakuwafukuza Wakanana walioishi Gezeri. Wakanana hao waliendelea kukaa kati ya watu wa Efuraimu mpaka leo, wakiwa watumwa wa kuwafanyia kazi za kulazimishwa.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan