Yoeli 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Yawe atashusha Roho wake 1 Kisha mambo hayo nitashusha Roho wangu juu ya watu wote. Watoto wenu wanaume na wabinti watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono. 2 Hata juu ya watumishi wanaume na wanawake, nitashusha Roho wangu wakati huo. 3 Nitafanya kitambulisho cha ajabu mbinguni na katika dunia; kutakuwa damu, moto na minara ya moshi. 4 Jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa kama damu, mbele ya kutimia kwa siku ya Yawe, siku inayokuwa kubwa na ya kutisha. 5 Halafu, watu wote watakaoomba kwa jina la Yawe wataokolewa. Katika mulima Sayuni na Yerusalema, kutakuwa watu watakaoponyoka, kama vile Yawe alivyosema: wale aliowachagua watabaki wazima. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo